Vyombo vya Habari Katoliki,vimewekwa ili kukabiliana na changamoto za ulimwengu mamboleo unaothamini zaidi habari za kiulimwengu.Kanisa linaishi ili kutimiza utume wake wa kiimani.
Ni kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu,Panama na Rais wa Baraza la Ushauri la vyombo vya Mawasiliano Katoliki,akivishukuru kwa kuwa vimekuwa kiunganishi katika kipindi cha karantini na mchango katika kuwaunganisha wananchi.
Akitoa shukrani zake za dhati, amevishukuru vyombo vya habari na kwa namna ya pekee kwa kazi za waandishi vilivyowavusha watu katika janga la virusi vya Corona na kudumisha umoja wa waamini.
Askofu OchogavĂa Barahona ametoa ujumbe huu kuhusu Vyombo vya Habari Katoliki, ambavyo vimewekwa ili kukabiliana na changamoto za ulimwengu mamboleo unaothamini zaidi habari za kiulimwengu.