Hofu pokot magharibi baada ya kiwango cha maji kuongezeka Turkwel

wakaazi wanaoishi karibu na bwawa la turkwel katika kaunti ya pokot magharibi  wameeleza wasiwasi kuhusu  kile wamesema  ni kuongezeka kwa kiwango cha maji  katika  bwawa hilo la turkwel kutokana na mvua kubwa ambayo inaendelea kushuhudiwa katika sehemu hiyo.

wakiongozwa na mama rose chepokwo wakaazi hao wamesema  bwawa hilo limefurika zaidi na huendaq  likavunja kingo zake iwapo  mvua itaendelea kunyesha .  kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la wazee eneo bunge la pokot kusini  anasema baadhi ya maafa  na mikasa ambayo  imekuwa ikishuhudiwa katika kaunti hiyo imekuwa ikitabiriwa tu na  wazee na  kutoa wito kwa serikali ya kitaifa  na  ya kaunti kuhakikisha kwamba  hatua za mapema zinachukuliwa ili  kuzuia   mikasa kama hii na  maafa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *