Walemavu walalamikia haki yao Kaunti ya Kajiado

watu wanaoishi na ulemavu katika  eneo la disil kaunti ya kajiado wanapanga kuandamana hadi katika afisi za  serikali zilizo mjini kajaido jumatano hii kushinikiza haki kutendeka  hasa katika utoaji wa msaada  wa serikali kwa watu wasiojiweza.

 kundi hilo la watu ambalo linaongozwa na samson kutoya wanasema licha ya machifu kutikwa jukumu la kuwaandisha wale wanapaswa kupewa msaada idadi kubwa ya watu wanaoishi na ulemavu  inaachwa nje na hivo wataandamana jumatano wakitaka watendewe haki. kadhalika wamemtaka kamishna wa kaunti ya kajiado   johnson  kanatha kuingilia kati na kuhakikisha  wanapewa misaada hiyo ikizingatiwa kwa sasa  wanapitia mahangaiko makubwa  na hali ngumu ambayo imesababishwa  na virusi vya  corona.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *