Magavana wataka Ugavi wa rasilimali kupitishwa na Seneti

Gavana wa Uasingishu Jackson Mandago na mwezake wa Elgeyio Marakwet Alex Tolgos  wamewataka maseneta kupitisha mfumo mpya wa ugavi wa rasmali za kitaifa kulingana na idadi ya watu katika kila kaunti  ili fedha zaidi zipelekwe maeneo ya mashinani.

Magavana hao wanasema kwamba mfumo huo  utasaidia  kaunti zilizo  na idadi kubwa ya watu kupata fedha za  kutosha  kutoa  huduma bora kwa mwananchi wa kawaida.

Naye gavana wa Busia Sospeter Ojamoong amelitaka bunge la Seneti  kupitisha mswada  wa ugavi wa fedha jinsi ilivyopendekezwa ikizingatiwa kaunti hiyo itanufaika  na mgao wa zaidi ya shillingi milioni 500

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *