Askofu wa jimbo katoliki la Eldoret askofu Dominic Kimengich, ametoa wito kwa wakristu kuomba mungu na kuwa tayari ili kumpokea roho mtakatifu.
Kwenye homilia yake katika kanisa la mama wa mitume seminary hapa mjini Eldoret, askofu Kimegich amesema kuwa hii leo ikiwa ni siku ya pentacoste wakristu wanapaswa kumuomba roho mtakatifu kuwasaidia kila wakati katika maisha yao.
Misa hiyo ilipeperushwa moja kwa moja na kituo hiki kwa lugha ya kalenjin.
