Askofu Kimengich; Sasa sio wakati wa siasa

Askofu wa jimbo Katoliki la Eldoret Rt. Rev. Dominic Kimengicha ametoa wito kwa viongozi nchini kusitisha malumbano ya kisiasa na badala yake kuelekeza juhudi zao katika kuangazia janga la Corona.

Kwenye homilia yake wakati wa Misa ya Jumapili ya kuadhimisha sherehe ya Kupaa Kwa Bwana katika kanisa la  Holy Family  Basilica  jijini Nairobi, askofu Kimengich amesema huu sio wakati wa viongozi kuanza kuzozana bali kuonyesha umoja wao katika kuwafaa wakenya wanaopitia wakati mgumu kiuchumi.

Askofu Kimengich amewataka  wanasiasa kuto tonesha vidonda vya uhasama wa kisiasa miongoni mwa wakenya kwa kuanza siasa za migawanyiko  sawia na zile zinazoshuhudiwa ndani ya chama cha Jubilee kuhusu nyadhifa za uwakilishi bungeni.

Wakati uo huo amewahimiza wakenya kutokata tamaa wakati huu wa janga la Corona bali kuendelea kumwomba Mungu ili kurejelea maisha yao ya kawaida  huku pia akiwatakia waislamu wote Eid-Mubarak.                                              

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *