Askofu wa jimbo katoliki la Eldoret amewahimiza wakristu kuwa na matumaini haswa wakati huu ambapo taifa linakumbana na janga la covid-19.Akizungumza na kituo hiki,askofu amewahimiza wakristo kuwa na imani dhabiti na kuendelea kumtumainia Mungu bila kuchoka .
Kulingana na Askofu,tumaini la taifa kwa sasa linatoka kwa Mungu,huku akiwahimiza wakristu kuwa na imani dhabiti.Anawakumbusha wakristu kutokua na vishawishi viovu haswa wakati huu wa changamoto nchini.