Papa Francisko azindua Mwaka wa 91 wa Mahakama ya Rufaa ya Kipapa

Papa Francisko amezindua Mwaka wa 91 wa Mahakama ya Rufaa ya Kipapa,akikazia juu ya haki na kuwawezesha udugu kwa wote hasa kulinda walio wadhaifu zaidi.

Ushauri wa Papa ni kuwa macho kwa ajili ya nafsi zao. Kwa  kufuata na kuwa na ushawishi mkubwa zaidi wa njia ya haki, kama njia ambayo inatoa  uwezekano wa udugu halisi na ambao kila mtu analindwa, hasa walio dhaifu zaidi, ndiyo umekuwa mwaliko wa Papa Francisko,alioutoa wakati wa kuzindua mwaka wa 91 wa Mahakama ya Rufaa ya Kipapa Vatican, mbele ya wahamasishaji wa Haki, wachunguzi, maafisa, wanasheria na wahudumu wa Mahakama

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *