Ikiwa ni jumapili ya tano ya mwaka wa kawaida katika kalenda ya kanisa,wito umetolewa kwa wakristu kuwa mwanga wa dunia. Katika homilia yake Padre David Kiptoo,ambaye ni msaidizi wa parokia ya Moyo mtakatifu wa Yesu kathedrali,amewaomba wakristo kuiga mfano bora na kuishi kikristu kama jinsi ilivyoratibiwa kwenye mafundisho ya kanisa.
Padre amekashifu wakristo ambao wanawahukumu wenzao kwa misingi mbalimbali huku akisema badala yake ni vyema kuwaombea.Akitoa mfano wa masomo ya siku,amewakumbusha wakristu kuwa wao ni chumvi na mwanga wa dunia.