ELDOWAS :ukosefu wa maji

Kampuni ya usambazaji maji   ya ELDOWAS kaunti ya Uasin Gishu imetangaza  kukosekana kwa huduma ya usambazaji wa maji kuanzia kesho  Jumatano saa tatu asubuhi hadi alhamis saa kumi na mbili jioni.

Kupitia notisi iliyotiwa sahihi na mkurugenzi wa kampuni ya eldowas peter biwott ameomba radhi kwa wakaazi akisema kuwa hali hii imechangiwa na  marekebisho ambayo yatafanywa na kampauni hiyo katika vyanzo vya maji vya chebara.

 Aliwaeleza wakaazi kuwa wakati marekebisho hayo yatakuwa yanaendelea sehemu ambazo hazijaathirika na ukarabati huu zitaendelea kupata usambazaji maji haya kama kawaida.

Wito umetolewa kwa wakaazi na sehemu ambazo zitaathirika kutafuta njia mbadala ya kupata maji  sehemu hizi zikiwemo kimumu, university of eldoret,marakwet farm , maili nne, munyaka, kapsoya, action,, rift valley bottlers, elgon view,  eldoret polytechnic,annex, langas, racecourse, ,chepkanga kapseret, marura, kamkunji, mwanzo, miongoni mwa zingine

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *