Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imefunga rasmi kampeni za chaguzi ndogo ambazo zitaandaliwa Jumanne, Disemba 15.
Kampeni hizo zilianza mnamo Oktoba 15 na kutamatika Jumamosi, Disemba 12, usiku wa manane.
Chaguzi ndogo zitaandaliwa Msambweni ambapo wakazi watamchagua mbunge wao, Kahawa Wendani, Kisumu Kaskazini, Lake View, Dabaso na Wundanyi wakazi watawachagua mawakilishi wadi wao.
Miongoni mwa viti ambavyo vinapiganiwa ni kiti cha ubunge cha Msambweni ambacho kiliwachwa kufuatia kifo cha Suleiman Dori ndicho kimevizia mirengo yote ya siasa
Kambi ya Niabu Rais William Ruto na ya Raila Odinga yalijaribu kupimajna nguvu yakiwapigia debe waniaji wao.