Meneja Akaidi “Curfew”

Maafisa wa polisi eneo la kesses wamewatia mbaroni  watu wanne akiwemo meneja  moja wa benki moja , afisa mmoja wa polisi  na mumiliki wa baa moja maarufu eneo la cheptret waliopatikana wamejifungia katika chumba cha kulala wakibugia pombe.

Wananchi eneo la cheptiret waliwawafahamisha  maafisa wa polisi kuhusu baa  ya eldorant ambayo  inasemekana imekuwa ikutumiwa na watu  wanaosafiri kutoka jijini Nairobi  ili kuendeleza unywaji pombe kinyume na maagizo ya serikali na wizara ya afya.

Wanne hao wamelazimishwa kusalia katika karantini ya lazima ya siku 14  eneo la kamalel.

 Kamishana wa kaunti ya uasingishu abdulzack jaldesa amesema kuwa sheria lazima itafuatwa haswa  kwa wale watakaokiuka masharti yaliyowerkwa wakati huu wa maanbukizi ya virusi vya corona.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *