Wito umetolewa kwa wazazi kuwaelekeza wanao na kuwapa malezi bora wakati huu wa janga la corona.
Akiongea na idhaa hii meneja wa bodi ya filamu katika kanda mwa kaskazini mwa bonde la ufa Emmanuel mbutu amewataka wazazi kutenga muda na wanao na kuwapa mwelekeo bora haswa utumizi wa mitanda ili wasipotoke kimaadili.
Amesema kuwa kutokana na utovu wa nidhamu unaoshudiwa nchini kutoka kwa baadhi ya watoto ni dhihirisho kamili kuwa wanafuatilia maswala ambayo hayastahili kwenye mitandao na pia vipindi kwenye runinga ambayo ni ya kuyapotosha.
Ameomba kila mtu kujukumika katika malezi ya watoto huku akisisitiza kuwa mtoto ni jamii nzima na hivyo kuwaongoza na kuwashauri kutawafaidi pakubwa wakati huu wammesalia nyumbani kutokana na janga la corona
hata hivyo amewataka washikadau katika sekta ya mziki, vyombo vya habari na sekta zi ngine kuhakikisha ule ujumbe unawafikia watoto ni wenyw maadili ya kukubalika katika jamii.
Aidha amewashauri watoto kuttumia uhuru wao kwa makini kwa kjiangazia upya ili wapate maisha bora siku za baadaye.