Tuwapime waliotangamana na Madereva wa Lori za masafa marefu

Wito umetolewa kwa serikali kuu kupitia wizara ya afya kupima watu wote wanaotangamana  na madereva   wa malori  ya masafa  marefu dhidi ya virusi vya corona.

Katika mahojiano na kituo kiimoja cha habari humu nchini, naibu gavana wa kaunti Uasingishu  Daniel Chemno ameshangazwa na jinsi vipimo hivi vinaendeshwa huku wanaotangamana na madereva hao wakisahaulika  bila ya kuzingatia hathari ya kusambaa wa virusi vya corona. ametaka wizara ya afya kuweka mikakati ya kutosha kuhakikisha ya kwamba  katika kila kituo ambacho  madereva hao husimama na kutangama   kila mtu amepimwa na kuthibitishwa iwapo ameambukizwa au la.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *