Serikali imeongeza makataa kwa wakenya wanao saka pasporti mpya hadi mwaka mmoja
Katika taarifa kwa vyombo vya habari kutoka kwa waziri wa usalama wa ndani Dr Fred Matiang’i walio na paspoti hiyo wana hadi tarehe mosi mwezi machi mwaka ujao kabla ya kuwacha kutumika rasmi
Amelalamikia idadi ya wakenya walio ugaibuni ambao hawajabadilisha pasporti zao akisema kwa sasa wako takriban milioni moja nukta nane. Matiang’i amesema ili kurahisisha kupata huduma hiyo serikali imebuni vituo katika kaunti za Nakuru, Uasin Gishu, Embu na Kisii huku zingine zikibuniwa katika miji ya Berlin, London, Paris, Washington DC, Johannesburg na Dubai.