kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa aden duale na mwenzake katika bunge la seneti kipchumba murkomen wamesema hawako tayari kupunguziwa mshahara kusaidia kuangazia changamoto za sasa za janga la covid-19.
wawili hao wanasema mshahara wanaopokea ni wa chini zaidi kutosheleza mahitaji ya fedha ya kitaifa kukabiliana na janga hilo la corona.
Wawili hao wanashinikiza kampuni kubwa zaidi nchini kuwa mstari wa mbele kusaidia katika kupambana na janga hilo.