Kasisi akashifu mauwaji kule Narok

Kasisi William Kapkiai  kutoka  kaunti ya Baringo amekashifu vikali mzozo  wa hivi karibuni wa kijamii katika kaunti ya Narok ambapo,watu wawili walipoteza maisha yao kwa mapigano uliotokana na kisa cha wizi wa mifugo.

Kasisi huyo ameongeza kuwa  kisa hicho cha Narok kusini inahujumu pakubwa umoja wa kijamii na kutaka viongozi wa eneohilo kuwa kwenye mstari wa mbele  kuhubiri amani, hasa baada ya kubainika kuwa mzozo huo  unahusiana  na umiliki wa ardhi baina ya jamii mbili za eneo hilo..

Akiongea katika eneo la Tenges  Kapkiai amewataka  Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake  William Ruto kutatua tofauti zao  hasa wakati huu  taifa ikikabiliana na janga la Korona.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *