Mwanamke mmoja kutoka kijiji cha Khwisero amefurushwa na mashemejiye ili kumzuia kurithi chochote kwenye boma hilo baada ya kukosa kufanikiwa kupata mtoto katika ndoa baada ya mumewe kufariki.
Millicent Aoko alikuwa amepewa notisi ya kuhama licha ya kuishi na mumewe zaidi ya miaka kumi iliyopita. Anadai licha ya chifu kujaribu kutatua mgogoro uliokuwa kati yao mashemejiye walifika na kubomoa nyumba yake huku wakibeba baadhi ya mali alioachiwa na mumewe.
