Utafiti feki

Gavana wa kaunti ya Uasin Gishu Jonathan Bii Chelilim amepuuzilia mbali  matokeo ya utafiti ulioorodhesha  serikali yake kuwa ya mwisho katika utendakazi nchini.

Kulingana na utafiti uliofanywa na kampuni moja ya utafiti ISS Africa – Kenya  kwa ushirikiano na  City Hub Limited,  kati ya tarehe 24 – 26 August, mwaka huu iliorodhesha  kaunti hii ya uasin gishu kuwa nambari arobaini na saba kati ya kaunti zote arobaini na saba.

Gavana bii amepuzilia mbali utafiti huo akisema kuwa matokeo hayo yalifadhiliwa na maasidi wake kisiasa akipongeza mkaguzi wa hesabu za serikali kubainisha Uasin Gishu ni miongoni mwa kaunti ambazo zilitumia fedha zao, uasingishu ikitumia asilimia 71.3 kwa fedha zilizotengewa maendeleo.

Kadhalika amewataka wapinzani wake kumuunga mkono katika juhudi zake za kutekeleze miradi ya maendeleo yanayonogeshwa kwenye nguzo yake kumi ya maendeleo aliyohaidi wakaazi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *