Gov Okoth Obado ajisalimisha

Gavana wa migori okoth obado amejisalimisha  asubuhi hii kwenye afisi za tume na maadili ya  kupambana na ufisadi  EACC.

Obado amejisalimisha katika afisi za eacc  kisii kuhojiwa kuhusu madai ya kufujwa kwa zaidi ya shillingi  million 73  pesa za umma.

Duru zinaarifu kwamba gavana Obado alifika katika afisi hizo akiwa pamoja na washukiwa wengine 9 wa kashfa ya ufisadi inayokumba  serikali ya kaunti ya Migori

hivi sasa Obado na washukiwa wenzake wanahojiwa na makachero wa EACC wakitarajiwa kuwasilishwa mahakamani baadaye.

Mkurugenzi wa mashtaka Nordin Haji  hiyo jana aliagiza akamatwe na kushtakiwa gavana Obado   pamoja na watoto wake wanne  na washukiwa wengine kuhusiana na kuporwa kwa mamillioni  ya pesa  kwenye serikali  ya kaunti ya Migori ambayo  Obado  anaongoza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *