Mbunge wa zamani wa Likoni Masoud Mwahima ameaga dunia nyumbani kwake Vyemani kaunti ndogo ya Likoni, Mombasa.
Kiongozi huyo wa zamani ambaye alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu Mbunge wa zamani wa Changamwe, Ramadhan Kajembe, alikata roho siku ya Jumatatu, Agosti 24, mwendo wa saa tano usiku.
Kulingana na familia yake, mwanasiasa huyo mkongwe aliaga dunia kutokana na matatizo ya pumu baada ya kupokea matibabu katika Hospitali ya St Thomas mnamo Jumapili.
Mwahima alichaguliwa mara ya kwanza kuwa mbunge mwaka 2007/2008 kupitia tiketi ya Chama cha Orange Democratic Movement (ODM) na kuchaguliwa kwa mara pili 2013 ambapo alihudumu hadi 2016 na kuondoka chama hicho na kuingia Jubilee.
Aliwania kiti hicho tena kuoiia tiketi ya Chama cha Jubilee Party wakati wa uchaguzi wa mwak 2017 lakini alipoteza kwa Mbunge wa sasa Mishi Mboko ambaye alishinda na tiketib yaODM.
Kabla ya kuchaguliwa kuwa Mbunge, Mwahima alihudumu kama diwani wa Shika Adabu, naibu meya wa Mombasa na kisha baadaye meya mwake 1999 hadi 2002. Pia aliwahi kuwa mwenyekiti wa KANU tawi la Likoni.
Wanasiasa wengi kupitia mtandao wa kijamii walimuomboleza mwanasiasa huyo. Kifo cha Mwahima kinakujia siku chache baada ya mwanasiasa mwingine wa Pwani Ramadhan Kajembe kuangamizwa na COVID-19.
