VICAR GENERAL :Jukumikeni katika kuwapa mwelekeo wanao

Padre mkuu wa jimbo katoliki la Eldoret William Kosgey amewataka wazazi kuwa karibu na wanao  msimu huu wa sherehe za krismasi.

Akihubiri katika  misa ya  kufunga mwaka ya wafanyikazi wa jimbo la Eldoret,Kosgey alisema kuwa msimu huu una majaribu na changamoto si haba na hivyo wajukumike kikamilifu katika kuwapa wanao mwelekeo ulio bora katika jamii.

Kadhalika aliwahimiza kutafakari safari yao ya ukristo na kumtukuza mungu wanapojitayarisha kumkaribisha yesu maishani mwao pindi tu atakapozaliwa na pia kunyosha mkono wa msaada kwa wengine ili wapate Baraka na uzima wa milele.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *